About Us

Ni blog iliyoanzishwa na Ms. Hadijah  Mdemu.  Mjasiriamali anayejishughulisha na shughuli mbalimbali za ujenzi na makazi hapa Tanzania; zikiwemo kazi zote za ujenzi  wa majengo katika hatua ya finishing kama vile uezekaji,upakaji, rangi,tiles,gypsum,makabati,milango,madirisha n.k!

 ‘ujenzinamakazitanzania’ ni blog inahusisha  shughuli zote za ujenzi na makazi hapa Tanzania. Ni blog inayohusisha wadau mbalimbali  wa sekta ya ujenzi kama vile Wizara ya ardhi ,Nyumba na Makazi;wakandarasi(Contractors) wachora ramani na wabunifu (Architects),wakadiriaji gharama za ujenzi  (Quantity surveyors),washauri(Consultants),wahandisi(Engineers),wasambazaji na wauzaji bidhaa za ujenzi,mafundi mbalimbali na pia wamiliki wa nyumba,majengo au ardhi.
Katika blog hii,utaweza kujionea  picha na matukio mbalimbali ya ujenzi na makazi; na pia utaweza  kupata maelezo mbalimbali yatakayokuwezesha  kujifunza mambo muhimu mbalimbali ikiwemo utendaji wa kazi tofauti za ujenzi

Blog pia itakupatia ufahamu au elimu mbalimbali ya sheria za ununuzi,umiliki ardhi,viwango vya malipo na mambo  muhimu ya kuzingatia  kabla na wakati wa ujenzi n.k!

Blog pia inatoa nafasi kwa wadau wote na  wasomaji,kutoa maoni yao,kutoa taarifa zozote muhimu zinazohisiana na ujenzi au makazi kama vile matatizo au kero zinazosababishwa na ujenzi holela.

Blog yetu  pia inatoa nafasi kwa wadau watakaopenda kutangaza kazi au biashara zao.

Zaidi ya yote,blog inakaribisha wamiliki wote  watakaopenda nyumba au majengo yao yaonyeshwe katika blog hii,kututumia picha hizo,na maelezo watakayotaka yaambatane na picha hizo,kufanya hivyo kupitia email yetu deco.tz@gmail.com  au kuwasiliana nasi kwa maelekezo zaidi kupitia namba  +255 713 175 966.